Na Happynus Pilula
Hakuna ninacho jivunia duniani zaidi ya kumjua Mungu, Huyo aliye baba yangu, anitulizaye wakati wote na kuniweka katika furaha yake.
Sina BABA mwingine ni wewe pekee pokeaa sifa na utukufu babaaaaaa,..... anipendaye kama wewe ni nani? Asiyetaka nipotee ni nani? Asiyechoshwa na udhaifu wangu ni nani? Anivumiliaye kuwa nitabadilika ni nani? Ni wewe pekee.
Tazama uliko nitoe, tazama nilipo, tazama wanaonizunguka hali zao na mienendo yao, je, leo hii nisingekuwa mmoja wao kama si huruma na upendo wako? Nakushukuru BABA
Wapo mafahari wengi wanapotea, wanashuka kuzimu kila siku. Zaidi ni vijana wenye nguvu wanaenda kuungana na Shetani. Baba naomba rehema zako juu yetu vijana. Tunapotea tunakwisha, tazama tunavyopukutika kwa uzinzi, uasherati, tamaa za mali, ujambazi. Baba nimekujia Wewe uliyetumaini na ngome yangu, msaada wangu wakati wa shida naomba usikie dua yangu na ukatuponye sisi tulio umbwa kwa mfano na sura yako, tuwe wa utukufu kwako, Tusilinajisi jina lako.
Zaidi bwana naomba mstari huu wa Isaya14:9-11 usiwe kimbilio letu vijana. Mahali petu pawe mbinguni paradiso. Tufurahi pamoja na wewe katika karamu ya Mwana kondoo.
"Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako,
Ili kukulaki utakapokuja;
Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako,
Naam, walio wakuu wote wa dunia;
Huwainua wafalme wote wa mataifa,
Watoke katika viti vyao vya enzi.
Hao wote watajibbu na kukuambia,
Je, wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi!
fahari yako imeshushwa hata kuzimu,
Na sauti ya vinanda vyako;
Funza wametandazwa chini yako,
Na vidudu vinakufunika.
NakupendaYesu, wewe ni Mzuri
Hakuna ninacho jivunia duniani zaidi ya kumjua Mungu, Huyo aliye baba yangu, anitulizaye wakati wote na kuniweka katika furaha yake.
Sina BABA mwingine ni wewe pekee pokeaa sifa na utukufu babaaaaaa,..... anipendaye kama wewe ni nani? Asiyetaka nipotee ni nani? Asiyechoshwa na udhaifu wangu ni nani? Anivumiliaye kuwa nitabadilika ni nani? Ni wewe pekee.
Tazama uliko nitoe, tazama nilipo, tazama wanaonizunguka hali zao na mienendo yao, je, leo hii nisingekuwa mmoja wao kama si huruma na upendo wako? Nakushukuru BABA
Wapo mafahari wengi wanapotea, wanashuka kuzimu kila siku. Zaidi ni vijana wenye nguvu wanaenda kuungana na Shetani. Baba naomba rehema zako juu yetu vijana. Tunapotea tunakwisha, tazama tunavyopukutika kwa uzinzi, uasherati, tamaa za mali, ujambazi. Baba nimekujia Wewe uliyetumaini na ngome yangu, msaada wangu wakati wa shida naomba usikie dua yangu na ukatuponye sisi tulio umbwa kwa mfano na sura yako, tuwe wa utukufu kwako, Tusilinajisi jina lako.
Zaidi bwana naomba mstari huu wa Isaya14:9-11 usiwe kimbilio letu vijana. Mahali petu pawe mbinguni paradiso. Tufurahi pamoja na wewe katika karamu ya Mwana kondoo.
"Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako,
Ili kukulaki utakapokuja;
Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako,
Naam, walio wakuu wote wa dunia;
Huwainua wafalme wote wa mataifa,
Watoke katika viti vyao vya enzi.
Hao wote watajibbu na kukuambia,
Je, wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi!
fahari yako imeshushwa hata kuzimu,
Na sauti ya vinanda vyako;
Funza wametandazwa chini yako,
Na vidudu vinakufunika.
NakupendaYesu, wewe ni Mzuri